Wagombea urais wagongana msiba wa Komba

Rais wa Tanzania,Jakaya Kikwete akiwafariji wanafamilia ya Mbunge wa Mbinga Magharibi na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Marehemu John Komba, nyumbani kwa marehemu Mbezi Tanki Bovu, Dar es salaam jana. Wapili kushoto ni Mke wa Marehemu. Picha na Said Khamis 
Na Fidelis Butahe, Mwananchi
SHARE THIS STORY

Dar es Salaam. Msiba wa Mbunge wa Mbinga Magharibi, Kapteni John Komba jana uligeuka uwanja wa siasa, baada ya makada wa CCM wanaotajwa kugombea urais pamoja na wapambe wao kupigana vikumbo na kurushiana vijembe, ikiwa na maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Ilikuwa kama walijipanga kwani kila mgombea aliyekuwa anafika katika msiba huo alionekana kuwa na wapambe waliompokea, kumpeleka kutoa pole kwa wafiwa na kumuonyesha eneo la kukaa.
Ukiacha kauli mbalimbali walizotoa kumwelezea marehemu Komba (61), wapambe wa wagombea hao walionekana mara kwa mara kuwa karibu nao wakizungumza, hali iliyoonyesha kuwa kila kundi lilitaka mgombea wao kuonyesha uwepo wake.
Waliohudhuria
Wanaotajwa kuutaka urais ambao walihudhuria msiba wa mbunge huyo uliotokea juzi jioni ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja, Mbunge wa Songea Mjini, Dk Emmanuel Nchimbi, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, wote kutoka CCM, pamoja na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibroad Slaa.
Wapiga picha na Membe
Membe ndiyo alikuwa wa kwanza kufika nyumbani kwa marehemu eneo la Mbezi Tangi Bovu na baada ya muda aliwasili Rais Jakaya Kikwete na kukaa naye.
Mara baada ya Rais Kikwete kuondoka, Membe alilakiwa na kundi kubwa la makada wa CCM ambao mbali na kumsalimia walimvuta pembeni na kuomba kupiga naye picha huku wakisika wakisema kuwa “Tunataka kupiga picha na mheshimiwa rais”.
Watu hao ambao walikuwa wakiongozwa na Mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Aden Rage ambaye hata hivyo hakupiga picha na waziri huyo, walisema kuwa kama mambo yakienda vyema, Membe anaweza kuwa rais na hata alipokuwa akiondoka walimsindikiza hadi kwenye gari lake.
Vijana na Nchimbi, Ngeleja
Ukiacha Dk Nchimbi ambaye alikuwa akizongwa zaidi na vijana wa CCM, kivutio kingine kilikuwa kwa Ngeleja ambaye mara kwa mara alikuwa akizungukwa na vijana waliokuwa wakimuuliza maswali mbalimbali, hasa kuhusu sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow.
Ngeleja pamoja na aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka walipata mgawo wa fedha kutoka katika akaunti hiyo na tayari wamehojiwa na Kamati Ndogo ya Maadili ya CCM, huku Ngeleja akisubiri kesho kuhojiwa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambayo tayari imeshamuhoji Profesa Tibaijuka.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment