Waliokiuka makubaliano ya Ukawa kuwajibishwa


Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyia Jumapili iliyopita. Kulia ni Naibu Mkurugenzi wa habari wa chama hicho, Abdul Kambaya. Picha na Rafael Lubava

Dar es Salaam. Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Freeman Mbowe amesema umoja huo utafanya tathmini ya maeneo ambayo wangeweza kushinda kwa kusimamisha mgombea mmoja kila eneo ili kuwachukulia hatua viongozi waliokiuka makubaliano hayo.
Wenyeviti wa umoja huo wa vyama vinne CUF, Chadema, NLD na NCCR Mageuzi, walisaini makubaliano kadhaa ikiwamo kusimamisha mgombea mmoja atakayeungwa mkono na Ukawa katika chaguzi zote kuanzia Serikali za Mitaa mpaka uchaguzi mkuu ujao.
Hata hivyo, katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Jumapili, katika baadhi ya maeneo, kila chama kilisimamisha mgombea wake na matokeo yake kuipa nafasi CCM kushinda.
Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema alisema viongozi wote kutoka vyama hivyo waliohusika kukiuka makubaliano hayo watachukuliwa hatua za kinidhamu.
“Tutafanya tathmini ambayo itatupatia picha halisi ya sababu zilizochangia baadhi ya maeneo kukiuka makubaliano. Tutawachukulia hatua za kinidhamu. Tunajua hawakuwa na maandalizi na muda wenyewe ulikuwa hautoshi lakini tutaangalia kwa nini hali hiyo ilijitokeza,” alisema Mbowe.
Mbowe alisema awali, viongozi wa ngazi za juu katika umoja huo walitoa maagizo ambayo yalitakiwa kutekelezwa na wagombea wote wanaounda Ukawa.
“Hakuna mwanachama asiyejua kama umoja ni nguvu, kwa viongozi wa ngazi za juu tunalifahamu hilo kwa kiwango kikubwa lakini hata ngazi za chini wanatakiwa kulitambua hilo,” alisema.
Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Mosena Nyambabe alisema changamoto hiyo imekuwa kikwazo ambacho kimesababisha kukosa ushindi katika maeneo mengi ya uchaguzi huo.
Nyambabe alisema tathmini itakayofanyika ndani ya umoja huo, itakuwa nafasi muhimu ya kujipanga kufanikiwa katika uchaguzi mkuu ujao.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment