Rajiv Gandhi: Waziri Mkuu wa kwanza kijana India


SHARE THIS STORY
0
Share
Rajiv Ratna Gandhi, alikuwa Waziri Mkuu wa sita wa India kutoka mwaka 1984 hadi 1989. Ghandhi alikuwa Waziri Mkuu kijana katika historia ya India, akichukua nafasi hiyo kutoka kwa mama yake, Indira Gandhi.
Indira, alikuwa binti wa Jawaharlal Nehru, aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza India kati ya 1947 hadi 1964, naye aliweka rekodi ya kuwa Waziri Mkuu wa kwanza mwanamke India.
Ukoo wa Jawaharlal Nehru una historia ndefu katika siasa za India, kutokana na ndugu wengi kushiriki siasa.
Hata baba yake Rajiv, Feroze alikuwa mwanachama wa Chama cha Indian National Congress. Bibi yake Rajiv, Kamala Nehru naye alikuwa mwanachama wa chama cha Allahabad.
Feroze na Indira walikuwa marafiki wa karibu wakati wanasoma Uingereza kabla ya kuja kuoana na kupata watoto wawili, Rajiv na Sanjay.
Rajiv aliuawa Agosti 20, 1944 kwa bomu la kujitoa muhanga Mei 21, 1991 wakati akiwa kwenye kampeni za uchaguzi. Mama yake pia (Indira) aliuawa kwa na walinzi wake.
Mwanzoni, Gandhi hakuwahi kuonekana kama mshirika wa mambo ya siasa, kwani fani yake kubwa ilikuwa urubani wa ndege.
Mwaka 1966, alirejea India baada ya kumaliza masomo ya urubani na kuajiriwa Shirika la Ndege la India. Mwaka 1968 alimuoa Antonia Maino, mwanamama aliyeanza naye uhusiano wakati akisoma Uingereza.
Baada ya kufunga ndoa, Maino alibadilisha jina na kuwa Sonia Gandhi. Rajiv alianza kujiingiza kwenye siasa kutokana na ushawishi wa mama yake baada ya kufariki ndugu yake Sanjay, aliyependa mambo ya siasa.
Rajiv alitangazwa kuwa Waziri Mkuu wa India saa chache baada ya mama yake aliyekuwa akishika cheo hicho, Indira Gandhi kuuawa Oktoba 31, mwaka 1984.
Utawala wa Rajiv ulianza kukumbwa na misukosuko siku chache baada ya kuapishwa baada ya kutokea vurugu zilizosababisha mamia ya watu kuuawa katika maandamano ya kuipinga jamii ya watu wa Sikh.
Katika kipindi chote cha utawala wake, Rajiv aliyekuwa Rais wa Chama cha Congress hakuwahi kuwa mbali na misukosuko hali iliyomfanya kutengeneza maadui wengi.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment