Bila kuondoa kasoro chaguzi Serikali za Mitaa, wapinzani ni wasindikizaji tu

SHARE THIS STORY
Share
Tukio kubwa linalotazamwa kwa umakini na wanasiasa wa Tanzania hivi sasa, ni Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Tayari Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imeshapuliza kipenga na kutangaza rasmi tarehe ya uchaguzi huo kuwa ni Desemba 14, mwaka huu.
Katika uchaguzi huo, vyama ambavyo vimekuwa vikipewa nafasi ya kuleta ushindani dhidi ya CCM katika uchaguzi huo ni CUF, Chadema na NCCR Mageuzi kutokana na msingi wake wa mashina katika ngazi za vijiji na vitongoji.
CCM imekuwa ikijigamba kuendeleza mtindo wake wa ushindi wa kishindo katika uchaguzi huo kwa kile inachodai kuwa na mtandao imara tangu katika ngazi za chini kabisa yaani mashinani.
Nini sababu ya vyama vya upinzani kuonekana kushindwa kufurukuta mbele ya CCM.
Pamoja na ukweli huo wa kujijenga katika ngazi za mashina, vyama hivyo vinalalamikia kuwepo kwa udhaifu mkubwa unaofanywa na Serikali kwa makusudi ili kuipa CCM fursa ya kuendelea kuwa na nguvu ya kuteka vijiji vingi nchini.
Nini kinaipa ushindi CCM
Samwel Ruhuza ni mdau wa masuala ya siasa. Amepata kuwa katibu mkuu wa NCCR Mageuzi Bara. Anataja moja ya kigezo kinachoipa CCM ushindi wa kishindo ni utaratibu uliopo wa uchaguzi huo kufanyika chini ya ofisi ya Waziri Mkuu ambayo inawakilishwa na wakurugenzi wa halmashauri za wiyala nchini.
“Wakurugenzi wa halmashauri ndiyo wasimamizi wa chaguzi hizo wanaowajibika kwa mkuu wa wilaya, ambaye ni mjumbe wa Kamati ya siasa ya CCM wilaya, kwa mazingira hayo kwa hakika ni asilimia ndogo sana CCM kukosa ushindi,” anasema na kuongeza:
“Mkuu wa wilaya ni mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi ya Wilaya anayetoa amri kwa mkuu wa polisi wa wilaya. Kwa hivyo CCM wanaweza kucheza ‘rafu’ za wizi na wasichukuliwe hatua kwa agizo la mkuu wa wilaya aliye na sura ya Mjumbe wa Kamati ya siasa (CCM).”
Ruhuza anatoa mfano wa hali iliyotokea Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma mwaka 1999 kuwa chama chake cha NCCR Mageuzi kilishinda katika vijijini vinane lakini Mkurugenzi wa halmashauri hiyo kwa kipindi hicho aliamua kufuta matokeo hayo.
“Nakumbuka kijiji kimojawapo ni Mvungwe, baada ya kunyang’anywa haki yetu tulikwenda mahakamani na kushinda mwaka 2003 ikiwa ni mwaka mmoja kabla ya kuingia uchaguzi mwingine 2004, licha ya usumbufu tulioupata, ile ilitujenga kisiasa na kutusaidia kushinda vijiji vyote uchaguzi uliofuata,” anaongeza Ruhuza.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment