YULE JAMAA AMBAE UVAMIA MASTAR KWENYE RED CARPET SASA MAHAKAMA YATOA UAMUZI

Screen Shot 2014-06-02 at 9.16.26 AMMovie mpya ya Angelina Jolie ( Maleficent) ni movie ambayo siku inaonyeshwa kwa mara ya kwanza wiki iliyopita kulitokea ishu ya Brad Pitt ambae ni mume wa Angelina Jolie kuvamiwa na kupigwa usoni na mtu yuleyule ambae amekua akihusishwa kuvamia mastaa kwenye red carpet kama Will Smith.
Screen Shot 2014-06-02 at 9.09.35 AM
Angelina kwenye movie yake mpya ya Maleficent
Brad hakuumia na badala yake aliendelea kukutana na mashabiki mbalimbali waliojitokeza huku aliemvamia akikamatwa na kupelekwa polisi ambapo taarifa mpya kuhusu huyu jamaa aliemshambulia Brad, ni kwamba atakua chini ya uangalizi kwa miaka mitatu na pia ameonywa kuwa anatakiwa kukaa mbali na shughuli za mastaa kwa umbali wa mita 457.
Show ambazo hatakiwi kujisogeza ni pamoja na uonyeshwaji wa movie pamoja na utolewaji wa tuzo na pia katika uangalizi wa miaka mitatu, Sediuk anatakiwa kufanya kazi za kijamii kwa siku 20.
Screen Shot 2014-06-02 at 9.28.25 AMSediuk pia ameonywa kukaa mbali kabisa na Angelina Jolie pamoja na Brad, vilevile atatakiwa kwenda kupata ushauri kutoka kwa wataalamu
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment