Tuliteleza mikataba ya madini, sasa tusonge mbele


SHARE THIS STORY
Tanzania ni taifa lililojaliwa madini mengi ya kila aina. Kitaalamu madini maana yake ni kitu chochote kinachokuwa katika mfumo wa kimiminika, kigumu (solid) au gesi ambacho ni cha kiasili kinachopatikana ardhini au chini ya bahari, maziwa, mito au kinapitia mfumo wa kijiologia lakini siyo mafuta au maji, kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 kifungu cha 4.
Madini ni vitu ambavyo vina thamani, hivyo kama yanasimamiwa vizuri yanakuwa na mchango mkubwa kwa maendeleo ya nchi.
Tanzania inatajwa kama nchi ya nne barani Afrika kwa kuzalisha madini kwa ujumla na ya tatu nyuma ya Afrika Kusini na Ghana kwa uzalishaji wa madini ya dhahabu. Madini mengine yanayochimbwa nchini ni pamoja na almasi, rubi, tanzanite na ulanga.
Katika uzalishaji huo, kuna baadhi ya migodi inamilikiwa na wachimbaji wadogo wazalendo na mingine inamilikiwa na wachimbaji wakubwa hususani makampuni ya kigeni na mingine inamilikiwa kwa ubia baina ya wageni na wazawa.
Serikali pia ina hisa katika baadhi ya migodi ya madini kupitia Shirika la Shirika la Madini la Taifa (Stamico).
Kupitia madini, mbali ya faida kama vile kutoa ajira kwa wananchi na kutoa bidhaa za kutumika migodini, pia Serikali inastahili kupata fedha nyingi kama mrabaha, na malipo ya kodi.
Mirabaha na kodi hizi hulipwa kwa mujibu wa sheria na mikataba iliyofikiwa baina ya Serikali na kampuni za uchimbaji madini.
Sheria na mikataba inapokuwa mizuri huipatia Serikali mapato makubwa, lakini sheria dhaifu na mikataba mibovu huipotezea nchi kipato, matokeo yake ni Taifa na wananchi wake kwa ujumla kuendelea kuwa duni kiuchumi licha ya kuwa na madini mengi.
Nguvu ya mikataba ya madini
Kwa mujibu wa sheria inayotumika ambayo ni Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na.14, ambayo ndiyo inayowaongoza kuhusu uchimbaji, utafutaji na usafirishaji wa madini, kimsingi mkataba wa madini unaingiwa kati ya mwekezaji kwa upande mmoja na waziri wa madini kwa upande mwingine. Waziri huyo huingia mkataba husika kwa niaba ya Watanzania wote.
Sheria imeweka mfano wa mkataba huo (sample agreement) chini ya tangazo la gazeti la Serikali na. 405 la tarehe 5/11/2010.
Kanuni ya 19 ya tangazo hilo inaruhusu Serikali kuboresha mfano huo wa mkataba kwa kuongeza vifungu au kifungu chochote wanachoona kinafaa.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment