Miaka mitatu ya kuchomwa kwa pasi na kung’atwa

Usiku wa Kuamkia Alhamisi ya Juni 5, binti huyo alifanikiwa kutoka katika ‘kifungo’. Majirani wa Amina ambao walishidwa kuendelea kuvumilia kusikia sauti za kilio cha Yusta mara kwa mara hasa nyakati za usiku.PICHA|MAKTABA 
SHARE THIS STORY

“Nilipofika tuliishi vizuri, lakini 2012 alibadilika na kuanza kuniadhibu, mara alinituhumu kutokufagia au kutopiga deki vizuri au chakula kuwa na chumvi nyingi. Mwanzoni alitumia fimbo alipohisi siumii alianza kuning’ata na kunichoma na pasi,” alisema.
“Alinikataza kulia kwa sauti na kunitisha kuwa ataniua au kuniroga nikimwambia mtu yeyote yale aliyokuwa ananifanyia.”
Yusta anasema kuwa tajiri yake huyo alibadilika zaidi baada ya kuondoka kwa mumewe ambaye hajui kama waliachana au alihama kikazi.
“Mwaka 2012 mumewe aliondoka na hapo ndipo matatizo yalizidi kwani hata mwanaye ambaye yuko kidato cha tatu alimpeleka shule ya bweni hivyo tulibaki wawili tu na hakukuwa na mtu wa kunisaidia,” anasema.
“Alinining’ata kila sehemu katika mwili wangu na alipoona damu imejaa mdomoni alitema na kisha kuendelea kuning’ata mpaka pale aliporidhika. Wakati mwingine alining’ata hadi usoni.”
Alisema alimfungia geti na kuondoka na funguo kila alipotoka kwenda kazini na alipomtuma sokoni alimuamuru kwenda haraka na kumkataza kuzungumza na mtu yoyote njiani hata majirani.
Aliongeza baada ya kuondoka kwa muwewe, Amina alikuwa na kawaida ya kwenda kwa waganga wa kienyeji na wakati mwingine waganga hao walifika nyumbani na kila walipofika alimfukuza na kumfungia chumbani hivyo hakujua walikuwa wakifanya nini.
Alitokaje kwenye kifungo
Usiku wa Kuamkia Alhamisi ya Juni 5, binti huyo alifanikiwa kutoka katika ‘kifungo’. Majirani wa Amina ambao walishidwa kuendelea kuvumilia kusikia sauti za kilio cha Yusta mara kwa mara hasa nyakati za usiku.
Majirani hao waliamua kupeleka taarifa za jambo hilo kwa taasisi isiyo ya kiserikali ya Jipange ambayo inafanya shughuli za kutetea wanawake. Baada ya kupata taarifa hizo, Jipange walitoa taarifa polisi na hapo ndipo mtego wa kumnasa Amina uliwekwa na hatimaye majira ya saa 8:00 usiku alikamatwa akiwa katika harakati za kukimbia na kumtorosha Yusta ili kuficha ushahidi.
Mwenyekiti wa Jipange, Janet Mawinza alisema walipopata taarifa za Yusta kutoka kwa wasamaria wema, waliwashirikisha polisi, lakini kwa bahati mbaya taarifa zilivuja na kumfikia mtuhumiwa hivyo alipanga njia ya kutoroka.
“Tulifika nyumbani kwa Amina majira ya usiku ili kulinda mtu asitoke, lakini kumbe yeye alishafahamu ujio wetu, hivyo aliruka dirisha na kukimbia. Alimkabidhi Yusta kwa kijana aliyetayarishwa kumtorosha.”
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment