Mabilioni yafyekwa safari za Kikwete

“Katika bajeti ya 2013/14 safari za Rais zilitengewa Sh15 bilioni lakini inaonekana fedha zilizotumika ni nyingi zaidi maana ndani ya miezi miwili tu zote zilikuwa zimemalizika,”.PICHA|MAKTABA 
Na Sharon Sauwa na Fidelis Butahe, Mwananchi
SharDodoma. Bajeti ya Sh50 bilioni zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya safari za Rais Jakaya Kikwete katika mwaka ujao wa fedha ni miongoni mwa mafungu ya fedha ‘yaliyopigwa panga’ ili kuwezesha kupatikana kwa fedha za kugharimia miradi ya maendeleo.
Habari kutoka ndani ya kikao cha majadiliano baina ya Serikali na Kamati ya Bunge ya Bajeti zinasema, Sh11 bilioni zimepunguzwa katika fungu hilo na kubakiza Sh39 bilioni.
Hata hivyo, kiasi kilichobakishwa ni ongezeko la asilimia 260 la Sh15 bilioni zilizopitishwa na Bunge mwaka jana kwa ajili ya safari za Rais katika mwaka wa fedha unaomalizika Juni 30 mwaka huu.
“Katika bajeti ya 2013/14 safari za Rais zilitengewa Sh15 bilioni lakini inaonekana fedha zilizotumika ni nyingi zaidi maana ndani ya miezi miwili tu zote zilikuwa zimemalizika,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Kwa hiyo kwa mwaka 2014/15 Serikali ilimtengea Rais Sh50 bilioni za safari, ila tumekata Sh11bilioni ili kupelekwa katika shughuli nyingine za maendeleo. Kwa hiyo kwa mwaka ujao wa fedha, safari za Rais zitatengewa Sh39 bilioni”.
Awali, ilielezwa kuwapo kwa mvutano mkali baina ya Serikali na Kamati ya Bunge ya Bajeti, lakini jana mchana pande hizo zilikubaliana kukata asilimia 7.5 ya fedha katika baadhi ya mafungu ya matumizi mengineyo (OC) kutoka katika wizara zote ili kuwezesha kupatikana kwa Sh230 bilioni ambazo zinahitajika kwa ajili ya maendeleo hasa katika sekta tatu; afya, miundombinu na kilimo.
“Bado kikao kinaendelea na tangu asubuhi tumekata fedha katika fungu la matumizi mengineyo, mfano chai katika ofisi za wizara pamoja na ununuzi wa magazeti, ununuzi wa magari ya kifahari, mafuta, viburudisho, semina na makongamano pamoja na safari za ndani,” kilieleza chanzo chetu.
Chanzo kingine kutoka Serikalini kilisema: “Katika siku ambazo tumevutana kwenye kikao cha kamati ni leo (jana), lakini mwishoni tulifikia mwafaka wa kukata kati ya asilimia saba na nane ya fedha za matumizi mengineyo katika wizara zote, ili kupata fedha za maendeleo.”
Juzi, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alisema wizara yake inakusudia kupitia bajeti za wizara zote ili kuhamisha fedha kutoka katika matumizi yasiyo ya lazima ili zielekezwe katika mahitaji muhimu.
“Kama wananchi wanakula mlo mmoja kwa siku, waliopo wizarani hawawezi kufa kwa kukosa chai asubuhi. Tutafanya hivyo ili fedha hizo zipelekwe katika shughuli za maendeleo.
Kesho (jana) katika kikao cha mashauriano tutakwenda kuweka msimamo wa pamoja katika jambo hilo. Wizara zisielekeze macho Wizara ya Fedha pekee, nazo zinatakiwa kuwa na mikakati ya kubana matumizi yake.”
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Andrew Chenge alipoulizwa kuhusu hatua iliyofikiwa katika majadiliano alisema: “Subirini itakaposomwa bajeti mtajua kilichoamuliwa.”
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment