Mifugo: Utajiri na ufukara kwa Watanzania

Takwimu za karibuni za Wizara ya Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi zinaonyesha kuwa Tanzania ina ng’ombe milioni 22.8, mbuzi milioni 15.6, kondoo milioni 7.0, kuku wa asili milioni 35.5, kuku wa kisasa milioni 24.5 na nguruwe milioni 2.01. 
Na Joseph Zablon, Mwananchi

Posted  Alhamisi,Novemba21  2013  saa 16:36 PM

Watu hawajadili tena uchumi, kila mtu yupo kwenye siasa na hiyo imesababisha kutouza mifugo au nyama katika Falme za Kiarabu.
Katika vijiji vya Wilaya ya Rufiji, Mkoa wa Pwani, vurugu zimekuwa zikizuka mara kwa mara na kusababisha nyumba za baadhi ya watendaji wa Serikali wakiwamo polisi kuchomwa moto.
Mali zinaharibiwa, watu wanapoteza maisha na wengine kubaki na ulemavu wa kudumu.
Ghasia hizo zinatajwa kusababishwa na kitendo cha mfugaji mmoja kutoka Kanda ya Ziwa kuingiza mifugo yake katika shamba la mkulima, mwenyeji wa eneo hilo na hata alipoulizwa, kulikoni, alipuuza. Mkulima huyo hakukata tamaa, badala yake alikwenda polisi kutoa taarifa ya mazao yake kuharibiwa na mifugo ambayo ilikuwa bado katika eneo la tukio, lakini hakuna askari aliyemjali wala kumsikiliza.
Mkulima huyo alirudi mbio hadi kijijini kwake na kuanza kupiga kelele za kuomba msaada, na kuwavuta wanakijiji wenzake, wakakusanyika kila mmoja akiwa na zana za mapambano na ghasia kubwa kuibuka.
Jeshi la Polisi lilitumia zaidi ya siku tatu kuzima ghasia hizo na hivyo kuigharimu Serikali fedha nyingi katika kuzima ghasia na gharama za matibabu.
Wakulima na wafugaji
Tikio hilo ni moja kati ya mengine mengi ambayo yanatokea katika maeneo mbalimbali nchini baina ya wakulima na wafugaji, ambayo yanawafanya wakulima kuwachukia wafugaji na kinyume chake. Tanzania, ikiwa nchi ya tatu kwa wingi wa mifugo barani Afrika ikitanguliwa na Sudan na Ethiopia, bado haijanufaika na mifugo hiyo.
Badala yake, mifugo hiyo inaonekana kuwa kero, karaha na chanzo cha umaskini na uvunjifu wa amani kuliko kuwa neema, furaha na chanzo cha utajiri.
Kwa wingi wa mifugo iliopo Tanzania, sekta hiyo ingetarajiwa kuinufaisha nchi na watu wake kwa kiwango kikubwa, jambo ambalo halijatokea.
Takwimu za karibuni za Wizara ya Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi zinaonyesha kuwa Tanzania ina ng’ombe milioni 22.8, mbuzi milioni 15.6, kondoo milioni 7.0, kuku wa asili milioni 35.5, kuku wa kisasa milioni 24.5 na nguruwe milioni 2.01.
Pamoja na mifugo hiyo, sekta hiyo imekuwa na mchango finyu katika Pato la Taifa (GDP), kwani katika kipindi cha mwaka 2011 ilichangia asilimia 3.7.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment