Ngassa atua Jangwani, asaini mkataba wa miaka miwili



Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrance Mwalusako (kushoto) akimkabidhi Mrisho Ngassa jezi wakati akimtambulisha rasmi jana, baada ya kusaini Yanga mkataba wa miaka miwili.Picha na Michael Matemanga 

Dar es Salaam.Wakati winga Mrisho Ngassa akisaini mkataba wa miaka miwili wa kuicheza Yanga, kiungo Haruna Niyonzima ametoa saa 24, kwa uongozi wa mabingwa hao kumalizana naye kabla ya kutimkia timu nyinginUongozi wa Yanga jana umemtambulisha rasmi Ngassa kumrejea kundini baada ya kumaliza mkataba wake na Azam ambao walimpeleka kwa mkopo Simba kwa muda wa mwaka mmojHabari ambazo Mwananchi ilizipata zimesema kuwa tayari uongozi wa Yanga umeshampa kitita cha Dola 10,000 kati ya Dola 30,000, mshambuliaji huyo ambaye aliondoka kwa mbwembwe kwenda Azam kwa dau la Sh50,000 milioChanzo hicho kimedai kuwa Ngassa bado anaidai klabu hiyo ya mtaa wa Jangwani kitita cha Dola 20,000 ambacho aliahidiwa kukabidhiwa mara atakapotua rasmi ndani ya klabu hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari Ngassa ambaye alikabidhiwa jezi iliyokuwa na jina lake na Katibu mkuu wa klabu hiyo Lwaurance Mwalusako alisema, “Namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kurudi tena Yanga, klabu ambayo nina mapenzi nayo
tangu utoto, nawashukuru viongozi wa Yanga waliopigana hasa rais Kifukwe (Francis) kuhakikisha wananirudisha kundini.
“Nilipokuwa Azam, Simba nilicheza kwa uaminifu mkubwa, lakini viongozi hawakuwa na imani na mimi kwa vile nina mapenzi na Yanga, ni kweli naipenda Yanga, lakini hata siku moja sikucheza kiuunazi, nilicheza kwa uaminifu kwa vile mpira ni ajira yangu, mapenzi yanafuata lakini viongozi hawakuliona hilo.
Kuhusu kusaini mkataba na Simba ambao alipewa dola 25,000 pamoja na gari aina ya Verosa Ngasa alisema “Sina mkataba na Simba na sijawahi kusaini mkataba na Simba, mkataba wangu ni Azam na Azam waliomnipeleka Simba kwa mkopo.
Akifafanua jambo hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Abdallah Binkreb alisema “Sh 25 milioni zilizotolewa na Simba ilikuwa ni ada ya kumtoa Azam kwenda Simba na gari alilopewa ilikuwa ni ushawishi tu ili akubali kucheza Simba klabu ambayo hakuwa na mapenzi nayo.”Naye
Akizungumzia suala hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zakaria Hanspop
alisema,“Mkataba wetu na Ngassa upo wazi tena unasema wazi utaanza pale ambapo mkataba wake na Azam utakapomalizika, hatujaingia mkataba juu ya mkataba kama Yanga wanavyodhani.
“Yanga wamezoea fujo wanafanya mambo kama vile TFF ni mali yao wanajua watabebwa, kwanza wao ndio waliomwambia Ngassa siyo mali kitu, ameshuka
thamani wakati ule sisi tulitaka kutoa milioni 20 wao wakaambiwa waongeze tano iwe sh 25 milioni ili wamchukue, walikataa na kusema hana thamani ya hela hiyo imekuwaje sasa? alisema kwa kuhoji.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment