Messi aishiwa hewa, atapika dimbani Bolivia



Kiungo wa timu ya taifa ya Argentina, Javier Mascherano akipumua kwa kutumia kifaa maalumu cha hewa ya oksijeni wakati wa mechi ya kuwania kufuzu kushiriki Fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Bolivia kwenye Uwanja wa  Hernando Siles Mjini La Paz, siku ya Jumanne. Picha na AFP. 


La Paz, Bolivia. Mbio za kufuzu kushiriki Kombe la Dunia nchini Brazil mwakani zimepamba moto katika mabara yote duniani.
Ukanda wa Amerika Kusini (Comebol), umekuwa kazini kwa mechi mbalimbali zilizochezwa karibuni, lakini iliyovuta zaidi hisia za wengi ilikuwa ni baina ya Argentina na Bolivia.
Kivutio kikubwa kilikuwa ni kwa Lionel Messi ambaye alishindwa kuona nyavu, aliugua ghafla, kuishiwa hewa na hatimaye kutapika uwanjani.
Ni nini kilichomponza?  Ni hali ya hewa katika mchezo huo ambao ulichezwa mjini La Paz, urefu wa mita 4000 kutoka usawa wa bahari. Huku, Messi mshambuliaji ambaye amefunga mabao 51 kwa klabu yake, Barcelona msimu huu, idadi ambayo ni pungufu ya mabao mawili kwa yale yaliyofungwa na gwiji Diego Maradona kwa nchi yake, Argentina aliishiwa nguvu.
Maradona ambaye siku hiyo alikuwa jukwaani mjini  La Paz, alimshuhudia Messi akiweweseka.
Mwenzake, winga Angel Di Maria naye pia alilazimika kupewa hewa safi ya oksijeni uwanjani katika mchezo huo ambao ulimalizika kwa sare ya 1-1.
Kwa kawaida, Bolivia hucheza mechi za nyumbani kwenye hewa hiyo dhaifu jijini La Paz, karibu mita 4,000 kutoka usawa wa bahari.
Hali hiyo huwaathiri wapinzani wao. Wataalamu wanaieleza hali hiyo kuwa huwapata wale wanaosafir urefu wa mita 2500 au zaidi kutoka usawa wa bahari.
Wanaongeza wataalamu hao kuwa hali hiyo inaweza kusababisha kuumwa kichwa, kukosa hamu ya kula na kichefuchefu (kuugua). Pia, kutapika, kujisikia uchovu mwingi, kizunguzungu au kichwa kuwa chepesi na kukosa usingizi.
Kwa watu wengi, dalili hizi zinaweza kupungua au kuondoka kwa kupumzika na kuizoea hali ile.  
Kuhusu tukio hilo la Bolivia na hali mbaya ya hewa, Messi alisema: “Ni hatari kucheza kule, kwa hiyo sare kwetu ni matokeo mazuri. Kila mara nilipojaribu kutembea na mpira kwa kasi, niliishiwa nguvu, sikuwa mwenyewe.
“Baadhi ya wenzangu walisikia maumivu ya kichwa, wengine walisikia uchovu, lakini mwanzo nilikuwa vizuri.”
Bao la Bolivia lilifungwa na Marcelo Martins  wakati bao la Argentina lilifungwa na Ever Banega.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment