Ulinzi mkali ibada ya Alhamisi Kuu D’Salaam

Paroko msaidizi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mwenyeheri Anwarite, Joseph Mapunda  akiwaosha miguu waumini wa kanisa hilo lililopo Makuburi wakati wa ibada ya  Alhamisi Kuu, jijini Dar es Salaam, jana


Dar es Salaam: Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Dar es Salaam Kardinali Polycarp Pengo  jana aliongoza ibada ya Alhamisi Kuu huku kukiwa na ulinzi mkali uliowajumuisha polisi waliovalia sare na wale kawaida, ikiwa ni siku moja baada askofu huyo kulituhumu jeshi hilo kwa kutowajibika ipasavyo.
Askari hao walikuwa wamegawanyika katika makundi mawili ambao baadhi yao walionekana wakirandaranda eneo la nje ya Jengo la Kanisa la Mt. Joseph ambako ibada hiyo ilifanyika huku wengi walikuwa ndani ya kanisa walikojumuika na waumini wa kawaida.
Haikuweza kufahamika mara moja sababu za kuimarishwa kwa hali ya ulinzi, lakini baadhi ya vyanzo vya habari vilieleza kuwa, hali hiyo imejitokeza kama sehemu ya kujaribu kukabiliana na hali yoyote hasa kutokana na vipeperushi vilivyosambazwa siku za chache zilizopita.
Pengo alikuwa akiendesha ibada ya Alhamisi Kuu ambayo Yesu Kristu alikuwa akifanya ibada hiyo kwa kuwaosha miguu mitume wake.
Ibada hiyo ilifanyika dunia nzima kwani hata Papa Francis alifanya kazi hiyo kwenye Makao Makuu ya Kanisa Katoliki kwenye Mji wa Vatican, Italia.
Siku chache kabla ya kuingia msimu wa Sikukuu ya Pasaka inayoanza leo kwa Ijumaa Kuu,
vilisambazwa vipeperushi vilivyokuwa na ujumbe wa kuvuruga ibada za Pasaka , hatua ambayo ilisababisha Jeshi la Polisi kutoa onyo kali dhidi ya jaribio lolote la uvunjifu wa amani.
Ibada ya Sikukuu ya Pasaka kitaifa imepangwa kufanyika mkoani Dodoma.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment