Arsenal yafungwa na Tottenham kwenye EPL.


256D4BC100000578-0-image-a-89_1423318735904

Tottenham Hotspurs wamefanikiwa kuwafunga Arsenal katika mchezo wa ligi kuu ya England uliopigwa hii leo (Jumamosi) kwenye uwanja wa White Hart Lane ukiwa mchezo wa kwanza wa ligi hiyo kwa ratiba ya jumamosi .
Arsenal ndio walianza mchezo huo kwa kasi zaidi wakipata bao la kwanza kupitia kwa kiungo mshambuliaji Mesut Ozil ambaye alifunga kwenye dakika ya 11  .
Spurs walisawazisha  bao hilo kupitia kwa mshambuliaji chipukizi Harry Kane ambaye alifunga kwenye dakika ya  56 ya mchezo zikiwa zimepita dakika 9 tangu kuanza kwanza kipindi cha pili .
Harry Kane akiifungia Tottenham bao la kusawazisha .
Harry Kane akiifungia Tottenham bao la kusawazisha .
Kane aliwahakikishia Tottenham pointi zote tatu kwenye dakika ya 86 kwa kufunga bao la pili bao ambalo limewapaisha Spurs mpaka kwenye nafasi ya 4 kwenye msimamo wa ligi kuu ya England.
Kane hadi sasa amefunga mabao 12 kwenye ligi hiyo ambapo anashika nafasi ya nne kwenye msimamo wa wafungaji akiwa nyuma ya Diego Costa , Sergio Aguerro  na Charlie Austin .
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment