ZOEZI LA UANDIKISHA WAPIGA KURA KIELEKTRONIKI (BVR), KWA MAJARIBIO LAANZA DAR



Zoezi la kuandikisha upya wapiga kura wenye sifa, kwa kutumia mfumo mpya wa kidigitali au kielektroniki, yaani Biometric Voters Registre, (BVR), limeanza jijini Dar es Salaam kwa majaribio, na hakika hakuna longolongo wala kupoteza muda, Mimi nimeshuhudia mtu mmoja humchukua takrivan dakika 10 tu kupatiwa kitambulisho au kadi ya kisasa ya kupigia kura. Hatua hizo ni kama zifuatazo, mosi, mtu anayeomba kuandikishwa ataonyesha kitambulisho na kujaza fomu ya Tume ya Uchaguzi ya kuomba kuaandikishwa, baada ya kujaza fomu hiyo hatua ya pili ni kuipeleka kwa muandikishaji msaidizi namba 2 ambaye ataingiza kumbukumbu hizo zilizomokatika fomu kwenye computer, hatua itakayofuata ambayo ni ya tatu, mtu huyo atatakiwa kuweka dole gumba na vidole vyake vitano ili viweze kuchukuliwa alama zake yaani scanned, baada ya hapo hatua inayofuata ni muombaji kupigwa picha na mwisho kabisa ni kupatiwa kikadi yaani kadi ya kupigia kura, kwa hakika inafanana sana na kitambulisho cha taifa, kama umekwishakipata. Zoezi hilo kwa mujibu wa tume ya taifa ya uchaguzi NEC, litaanza rasmi nchi nzima kuanzia Februari mwaka 2015 ambao ndio mwaka wa uchaguzi mkuu
Mwandishi msaidizi wa Tume ya Uchaguzi ya Taifa, (NEC), ambaye kwa sasa watajulikana kama BVR Operators, akijaza fomu ya mtu anayeomba kuandikiswa kupiga kura leo Jumanne Desemba 16, 2014, plae Bunju A, wilaya ya Kinondoni jimbo la Kawe jijini Dar es Salaam
Muombaji (Kulia), akijaziwa fomu kabla ya kuendelea na hatua zingine
Muombaji (Kulia), akikabidhi fomu aliyojaziwa katika hatua ya kwanza ya kuomba kuandikiswa
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment