D'BANJ AMZAWADIA RAIS WAKE WA NIGERIA ZAWADI HII YA CHRISTMAS

Beats By Dre
Dapo Daniel Oyebanjo a.k.a D’Banj amekuwa Balozi wa bidhaa za Beats by Dre kwa upande wa Afrika kwa miezi kadhaa sasa, dili linalomfanya aongeze ile mirija ya kujaza akaunti zake za Benki Naira nyingi tu kila mwezi.
Beats by Dre zina heshima yake kubwa sokoni kwa sasa, najua unajua hilo, kingine ni kwamba kuna zile special ambazo huwa zinatengenezwa chache na maalum kabisa, mtu ambaye anaweza kupewa labda ni Balozi wao au mtu mwingine maalum kama zawadi, kama ikitokea zikiuzwa basi bei yake huwa ni bei maalum vilevile.
Katika zile special ambazo zimewahi kutolewa kwa Balozi D’Banj, aliwahi kumpa zawadi ya aina hiyo Iyanya wakiwa Airport Nigeria, baada ya hizo taarifa ikufikie kwamba safari hii zali hilo limemuangukia Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan.
Kaweka picha Instagram (iambangalee) akimvalisha Mr. President mzigo huo, mitandao ya Naija haikukosa neno, wanasema eti Rais alionekana kama hakuipokea poa hii ya kuvalishwa headphone hizo, huenda Balozi huyo alikiuka protocol labda.
Aliandika hivi kwenye post hiyo; “Merry Christmas Mr President with Love from@iambangalee and @Beatsbydre OooSssHhhEee“– @iambangalee
Cheki tukio zima hapa.
DBanj-600x600
17-564x372
DBanj1-600x600
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment