Kashfa nzito sekta ya afya

Tayari Mfuko wa Kimataifa unaoshughulikia Ugonjwa wa Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria wa Global Fund, Shirika lisilo la Serikali linalojihusisha na masuala ya afya (Sikika) na watumiaji wa ARV nchini wamethibitisha kuwapo kwa upungufu huo na hatari zake kiafya kwa wagonjwa.
SHARE THIS STORY
Maisha ya baadhi ya watu wanaotumia dawa za kufubaza makali ya ugonjwa wa Ukimwi (ARVs), yapo hatarini, baada ya kupungua kwa dawa hizo nchini na hivyo kufanya wagonjwa kutumia dawa tofauti na zile wanazotumia siku zote.
Uchunguzi wa gazeti hili umegundua kuwa hali hiyo inatokana na urasimu wa baadhi ya taasisi za Serikali, ambazo zinachelewa kuagiza dawa za ARVs kwenye viwanda vya nje ya nchi.
Tayari Mfuko wa Kimataifa unaoshughulikia Ugonjwa wa Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria wa Global Fund, Shirika lisilo la Serikali linalojihusisha na masuala ya afya (Sikika) na watumiaji wa ARV nchini wamethibitisha kuwapo kwa upungufu huo na hatari zake kiafya kwa wagonjwa.
Global Fund katika ripoti yake ya robo ya mwaka huu (Januari- Machi), imekiri kuwapo kwa upungufu wa dawa za ARV nchini na athari ambazo wameanza kupata wagonjwa.
Ripoti hiyo inaonyesha upungufu huo wa dawa za ARV unatokana na uzembe wa baadhi ya taasisi za Serikali kuchelewa kuagiza dawa hizo pamoja na kuwapo kwa mabadiliko katika ununuaji na ucheleweshwaji wa kupatikana fedha za kununulia ambao umesababisha upungufu huo.
Taarifa hiyo inaeleza kuwa waathirika wakuu katika upungufu huo wa dawa ni wanawake wajawazito wanaoishi na virusi vya Ukimwi, ambao wanatakiwa kutumia ARV aina ya TLE ili kuzuia maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto.
Upungufu huo, umesababisha wagonjwa kubadilishiwa dawa tofauti na zile wanazotumia hali ambayo imesababisha baadhi yao kinga ya mwili (CD4) kushuka.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika baadhi ya mikoa nchini unaonyesha tatizo hilo la kupungua kwa ARVs nchini, limewaumiza wagonjwa wengi na kwamba sasa wanapokwenda hospitali wanapewa dawa za kutumia wiki mbili au vidonge 10 badala ya dawa za mwezi mmoja au miwili.
Sikika
Shirika lisilo la Kiserikali (Sikika), linalojihusisha na masula ya afya, wamebaini kuwapo kwa upungufu wa dawa za ARV katika mikoa ya Kigoma, Kilimanjaro, Tabora, Shinyanga, Morogoro, na Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Sikika, Irenei Kiria alimwambia mwandishi wa gazeti hili kuwa taarifa walizozipata kutoka kwa watu wanaotumia ARV, upungufu mkubwa wa dawa hizo kwa Mkoa wa Dar es Salaam upo katika katika Hospitali za Mnazi Mmoja, Mwananyamala, Amana na Temeke.
Katika hospitali hizo wagonjwa wanabadilishiwa dawa za ARV na kupewa tofauti na zile ambazo wamezoea kuzitumia.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment