Wizkid na P-Square waondolewa kweye kinyang'anyiro MTV EMA 2013

Kwa mara ya pili mfululizo, wasanii wa Nigeria wanaowania Tuzo za MTV katika category ya Africa wameondolewa katika mashindano hayo.
Waandaaji wa Tuzo hizo wametangaza kuwa wasanii wa South Africa, LCNVL wamepigiwa kura kama Best African Act, position iliyowaondoa WizKid na P-Square katika mashndano hayo. Mwaka jana Wizkid na D'banj walikuwa ni washiriki pia kutoka Nigeria ambao hawakupita pia.
Kwa wiki sita zilizopita MTV waliwapa mashabiki nafasi ya kupiga kura kwa wasanii wao wa nyumbani wanaowapenda kuwasaidia kupata "The Best Act" tittle kupitia wao. LCNVL sasa wamesogea katika hatua ya pili ya kupigiwa kura ili kujaribu kupata nafasi ya kuwakilisha wanapotoka katika World Wide Act category katika Tuzo hizo zitakazo fanyika siku ya jumapili, ya November 10, Amsterdam.
LCNVL inayoundwa na mapacha wawili, Brian na Andrew Chaplin  wamekuwa ni wasanii maarufu na wenye mafanikio makubwa nchini SA kwa miaka 5 sasa, wakiwa wameuza zaidi ya copy 100,000 ya album zao, wameshinda Tuzo za SAMA (South African Music Awards) kama album iliyouza sana tuzo ya wasanii wapya (Best Newcomer) na kufanya tua duniani wakiwa na Justin Bieber, Tiao Cruz, Mike Poser na Jason Darulo.
kuanzia sasa LCNVL watachuana na Honey Singh (India) na Ahmed Soultan (MIddle East) katika nafasi ya 10 bora watakaoingia katika category ya  Worldwide Act.
Ripoti zinadai kuwa Miley Cyrus, Robin Thicke, Snoop Dogg, Afrojack, Imagine Dragons, The Killers na Katy Perry wanategemewa ku-perform katika MTV EMA 2013.
Hivi karibuni Wizkid ameachia video ya wimbo wake "Jaiye jaiye" itizame hapo chini
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment