Rapper maarufu South Africa anusurika kuuwawa na polisi kimakosa

Rapper maarufu South Africa na mshindi wa tuzo kadhaa, amekoswa koswa kuuwawa baada ya kurushiwa risasi kadhaa na polisi Johannesburg asubuhi ya leo wakidhani ni mshukiwa wa utekaji nyara.
Khuli Chana ambae jina lake halisi ni Khulane Morule, alikuwa amesimama katika kituo cha mafuta akitaka kujaza mafuta kwa ajili ya kuelekea Pretoria kwa ajili ya kufanya show, kwa bahati mbaya ikatokea kuwa kituo alichokuwepo ndio hicho kilichochaguliwa kama ni sehem ya kitovu cha uhalifu huo.

Polisi waliokuwepo katika eneo hilo waliarifiwa kuangalia gari ya kijivu aina ya BMW kama gari la mtekaji nyara huyo.Chana alikuwa akiendesha BMW yenye rangi ya blue wakati huo, na baada ya kutokusimama katika eneo la polisi ambalo halikuwa rasmi, gari la Rapper huyo, lilirushiwa risasi 6 za onyo, Chana alipatwa na risasi katika kidole na mgongoni, ambapo saa hii anaugulia nyumbani kwake baada ya kuruhusiwa hospitali.
"Ukweli wa mambo huu ni ukatili wa polisi," amesema Manager wa Chana Refiloe Ramogase. " Polisi wanahitaji kuwa na tahadhari zaidi kabla ya kutumia nguvu ya kuuwa."
Tukio hilo kwasasa linachunguzwa na Independet Police Investigative Directorate.
Chana aliondoka na tuzo 3 za tuzo za mziki wa South Africa mwezi wa 5 ikiwemo albam bora ya mwaka "Lost in Time" ikiwa ni maraya kwanza kwa msanii wa Hiphop kuchukua tuzo hiyo katika historia ya tuzo hizo zilizoanzishwa miaka 19 iliyopita.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment