“MUZIKI GANI”- NEY WA MITEGO Feat. DIAMOND (BONGO FLEVA Vs BONGO HIP HOP-NANI ZAIDI?)






vcd
Kwangu mimi binafsi, muziki ni muziki. Of course ninazo aina za muziki zinazonivutia kushinda zingine. Na pia zipo aina za muziki ambazo sivutiwi nazo kabisa…punk rock kwa mfano. Lakini mwisho wa siku naheshimu kila kazi ya ubunifu na ndio maana nasikiliza kila aina ya muziki. Ukifanikiwa kushika iPod yangu utakuta nina kila aina ya muziki.Charanga,Country,Rock,Pop…you name it.
Hata hivyo, linapokuja suala la muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania, nina chaguo langu pia…well…tulia..napenda kila aina ya muziki toka Bongo. Wewe Je?…Kuna Hip Hop na kuna Bongo Fleva. Diamond anaimba Bongo Fleva na Ney Wa Mitego anaondoka na Bongo Hip Hop.
SONG: MUZIKI GANI
ARTIST: NEY WAMITEGO FEAT DIAMOND
PRODUCER: MR TOUCH
 
CHORUS
Hivi nyi ma mc mnachoimba kitu gani, mara bangi mara matusi sa ndo muziki gani (diamond).
Hii no hip-hop h.o.p muasisi wa burudani, tushachoshwa kutwa mapenzi, kabane Pua nyumbani (ney)  X2
 
DIAMOND
Hata bibi yangu mi aliniambia , mwanamke anahitaji kubembelezwa
Kupetipeti matunzo pia, ukienda rafu utampoteza,
Muziki ni mfano wa binti muzuri,
Na ndio maana namtunza kwa   vazi na uturi
 
NEY WA MITEGO
Aaah piga kimya, we ndo haufai kabisa hauna maana
Wabana pua kila siku mnarogana, bibi yako alikuambia muziki ni kama binti
Mbona unawachezea unawatema kama big g
Mara wema, mara Jo keti, mara Naj, mara Penny, je mnafanya mziki mpate mabinti
 
DIAMOND
Uuuhhuuuu, hata wazee wazamani, walishasemaga kazi na dawa
Chamuhimu jukwaani, ni kuhakikisha wanapagawa,
Kwa michezo ya kuringa ringa  ndo huwa wanadata
Badilika usiwe mjinga, utawakamata
 
CHORUS
Hivi nyi ma mc mnachoimba kitu gani, mara bangi mara matusi sa ndo muziki gani (diamond).
Hii no hip-hop h.o.p muasisi wa burudani, tushachoshwa kutwa mapenzi, kabane Pua nyumbani (ney)  X2
NEY WA MITEGO
Muziki wenu ushirikina ndio umetawala, q chilla analalama anasema umemroga
 Mganga wako aliekutoa umemkimbia hujalipa,  bila skendo za magazeti basi huskiki
 
DIAMOND
Mi ni mti wenye matunda, milele siogopi kupigwa mawe
Ubaya wenu wengi kayumba, elimu mliitupa sandakalawe
 
NEY WA MITEGO
Bado hujanishawishi, bongo fleva inanipa kichefu chefu
Kwanza nyie malimbukeni wa umaarufu
Mnalenta maringo mpaka kwa mashabiki , Wabana pua nyie watoto sio riziki,
Mnavaa nguo za dada zenu, zinawabana mapaja nyie makaka duu
Aah nyie watoto mchele mchele , kwenye show viuno mbele mbele X2
Nimewanyamazisha, brazameni vipi  we bado unabisha
 
DIAMOND
Mi nnamengi nnayajua, ila we ni mtemi utaanzisha utata
Michezo yenu kutoboa pua, bora ninyamaze usinipige mbata
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment