AMAZON 'AJITOA' MTANASHATI ENTERTAINMENTS

Staa wa singo ya 'Mamito' ambayo iko juu hivi sasa kwenye vituo kadhaa vya redio hapa Bongo, Justin Kobelo 'Amazon' ametangaza rasmi kujiondoa kwenye kundi la Mtanashati Entainments linaloongozwa na Ostaz Juma na Musoma kwa kile alichokiita ubabaisha katika masuala ya uongozi na mikataba ya kazi.
Amazon amefunguka kuwa tangu kujunga na kundi hilo hakuwahi kupatiwa fursa ya kurekodi nyimbo yoyote mpya achilia mbali Checherumba ambayo amearifu kuwa aliirekodi kabla ya kujiunga na kundi hilo.
"Yaa! ni kweli kuwa nimeamua kuondoka Mtanashati kuepuka ubabaishaji mkubwa uliopo ndani ya kundi hilo ambalo mkurugenzi wake amekuwa akiwanyima nafasi wasanii wengine na kuwapendelea baadhi akilenga zaidi kujinufaisha kupitia majina ya wasanii hao" alisema Amazon
Akiendelea zaidi nyota huyo wa singo ya checherumba alisema kuwa amechoshwa na 'uditeta' wa mkurugenzi unaofanywa na mkurugenzi wa kundi hilo ikiwemo hatua ya kuwataka wasanii walio ndani ya kundi hilo kutia saini mkataba wa Milele utakaowafanya kuwajibika ndani ya kampuni hiyo maisha yao yote.
"Awali nilitakiwa kusaini mkataba wa 'milele' ambao unakutaka kufanya kazi maisha yako yote ndani ya kundi kitu ambacho binafsi nilikitaa kwa kuwa sijawahi kuona mkataba wa aina hiyo sehemu yoyote ile ingawa ajabu ni kuwa kuna baadhi ya wasanii wenzangu wameukubari" alisema Amazon.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment