Shivji auponda mchakato Katiba Mpya

Mwanazuoni na  Mwanasheria nguli, Profesa Issa Shivji. 

Asema umehodhiwa na wanasiasa na kutahadharisha usipoangaliwa unaweza kuzaa machafuko.
Dodoma.  Mwanazuoni na  Mwanasheria nguli, Profesa Issa Shivji  ameuponda mchakato wa Katiba Mpya kuwa umehodhiwa na wanasiasa na kutahadharisha kuwa usipoangaliwa vizuri unaweza kusababisha machafuko.
Aliyasema hayo jana mjini hapa alipokuwa akitoa mhadhara kwa Jumuiya ya Chuo Kikuu cha Dodoma, (Udom). Mhadhara huo uliandaliwa kama sehemu ya mafunzo kwa ajili ya wanafunzi wanaojiandaa kuhitimu masomo yao (Convocation ).
Profesa Shiviji ambaye alitumia saa 1.15 kutoa mhadhara wake juu ya mchakato wa Katiba, alisema Bunge la Katiba lipo juu ya Bunge la Kawaida.
Alisema katika historia ya Tanzania imewahi kuwa na mabunge mawili yaliyoandaliwa kupata Katiba, lakini yote hayakuwa na wabunge waliochaguliwa.
“Tukiangalia katika historia hatukuwahi kuwa na Bunge la Katiba ambalo lilichaguliwa na wananchi. Safari hii tulikuwa na nafasi ya kuwa na Bunge ambalo lilichaguliwa na wananchi lakini kwa bahati mbaya hakuna nafasi ya kufanya hivyo ,”alisema.
Kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, wabunge wote 357 na Wawakilishi 81 watakuwa ni wabunge wa Bunge Maalumu la Katiba huku mashirika yasiyo ya kiserikali yakipewa wawakilishi 20.
Wajumbe wengine ni vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu 42, wawakilishi wa taasisi za elimu ya Juu 20, watu wenye mahitaji maalumu (20), vyama vya wafanyakazi (20), wafugaji (10), wavuvi (10), wakulima (20) na makundi mengine yenye mahitaji muhimu ni wawakilishi (20).
Profesa  Shivji  alisema Bunge la Katiba litakuwa na jumla ya wabunge  639, ambapo 438 asilimia 69  ya wabunge wa Bunge hilo wanatokana na vyama vya siasa.
Alisema kati ya wabunge hao kutoka vyama vya siasa asilimia  52 ni Wana-CCM na asilimia 16  ni kutoka vyama vya upinzani.
“Katika wajumbe 42 watatokana na vyama vya kisiasa, kwa hivi itafanya jumla ya wabunge la Katiba ambao watatokana na vyama vya siasa kuwa ni asilimia 75;
“Kama hesabu zangu ni sahihi ama zinakaribia wabunge wanaotokana na CCM watakuwa ni  asilimia 63, wapinzani asilimia 27 na wasiokuwa na chama ni asilimia 10,”alisema.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment