Viboko wa ajabu wasiojulikana kwa watalii

 


Wakazi wa kijiji hicho chenye wakazi wapatao 1525 wanaotokana na makabila ya Wamwera, Wangindo, Wamakonde, na Wamachinga ambao wanalitumia eneo hilo kama kivutio cha utalii ambalo linachangia pato la wakazi wa eneo hilo mpaka taifa kutokana na watalii wa ndani na nje.
Viboko wa ajabu
Katika Kijiji cha Makangaga, kilometa tisa kutoka kijijini hapo, kuna Mto Nyange uliosheheni viboko wa ajabu ambao wana tabia ya ‘kucheka’ na kutii amri zinazotolewa, hakika ukifika unajua wamefundishwa, ni fursa nzuri ya utalii kama itatumiwa vyema.
Majira ya usiku viboko hao wanapenda kutembea kando ya maeneo yao kwa ajili ya kujipatia vyakula na sehemu kubwa wanakula majani na pia wana tabia za ziada.
Zaidi ya miaka 100 iliyopita mto huo uliotengeneza bwawa na haukuwa na kiboko hata mmoja, wakazi wa maeneo hayo walitumia bwawa hilo kwa shughuli za uvuvi na mahitaji ya maji kwa kazi za kawaida.
Mkazi wa eneo hilo Yahaya Selemani Engema anaeleza chanzo ni mkazi mmoja aliyetajwa kwa jina la Kimombo ambaye alikuwa mvuvi hodari kwenye bwawa hilo.
Lakini siku moja alipokwenda kuvua hakurejea na historia kuanzia hapo baada ya wananchi kuona kiboko mmoja kwenye bwawa hilo.
“Ndugu zake baada ya kusubiri kwa siku sita wakiamini atarejea, waliamua kwenda bwawani hapo kwa nia ya kumtafuta, walimwita kwa kutumia lugha ya kabila la Wamachinga, ajabu baada ya kutokea Kimombo kama walivyotarajia alitokea kiboko ambaye alicheka kama ishara ya kuitika, kutokana na hali hiyo ndugu wa familia ya mvuvi huyo waliamini ndugu yao alizama kwenye bwawa hilo na kubadilika kuwa kiboko ambao wanatabia ya kucheka,”anasema Omari Yanda mmoja wazee maarufu kijiini hapo.
Kila mwaka hivi sasa inakadiriwa kuwa wanafikia zaidi ya viboko 300, na kwamba wanatii amri ya ukoo wa Kimombo.
“Familia iliyoshikilia wanyama hao ni ya Kimombo wanarithishana kwa kuwa kiboko wa kwanza alitoka katika familia hiyo, wageni wanaofika kuwaona viboko hao huwaita viboko hao kwa kutumia jina la Kimombo ndipo viboko hao hujitokeza wakicheka,” anasema Yanda.
Miongoni mwa maajabu ya viboko hao ni kuwa wana uwezo wa kujitokeza pindi wanapohitajika kwa maana wakitakiwa wajitokeze wadogo wataibuka wadogo na wakitakiwa wajitokeze wazee watajitokeza wazee wote waliomo bwawani.

SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment