SIRI ZAIDI ZA KIFO CHA MWANAMUSIKI LANGA

Na Mwandishi Wetu
MWILI wa mwanamuziki Langa Kileo jana (Jumatatu) ulipumzishwa kwenye nyumba ya milele katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar lakini nyuma ya kifo chake kuna siri ambayo rafiki yake wa karibu (jina linahifadhiwa) mkazi wa Mikocheni A jijini Dar ameamua kuiweka hadharani.
Akizungumza na Uwazi juzi, rafiki huyo wa marehemu alisema, siku chache kabla ya kifo chake alimfuata na kumwambia kuwa Israel mtoa roho anamtembelea usiku na anahisi siku si nyingi atamfuata mshikaji wake aliyetangulia mbele ya haki, Albert Mangweha ‘Ngwea’.
“Hii ni siri ambayo hata ndugu zake hawaijui lakini mshikaji alijua anakufa. Alijitahidi kukikwepa kifo lakini alishindwa. Siku chache kabla hajafa, usiku alikuja kwangu na kuniambia kule kwao kwenye geto lake analoishi ambalo liko ghorofani, anaona mauzauza na anahisi kifo kinamuita.
“Nilishangazwa sana na maneno yale. Akazidi kuniambia eti kwa jinsi mambo yanavyokwenda hawezi kuendelea kulala kwao na kuanzia siku ile angelala na mshikaji wetu mwingine pale Geza, Mikocheni A.
“Kweli siku hiyo alilala pale akiwa na hofu kubwa na asubuhi baadhi ya watu wakawa wanamshangaa akiwa ‘amezima’ nje ya lile geto la mshikaji wake. Alivyoondoka sikumuona tena mpaka nilipokuja kuambiwa yuko hoi kwa malaria na kesho yake nikasikia hatunaye, nimeumia sana,” alisema mtoa habari huyo.
Alipoulizwa juu ya uhusiano wa kifo cha Langa na matumizi ya madawa ya kulevya, rafiki huyo alisema: “Inaweza ikawa ngumu kwa ndugu wa marehemu kuhusisha kifo chake na madawa ya kulevya lakini mimi namjua Langa nje ndani, ukweli ni kwamba jamaa alikuwa akiendelea kula ‘mambo’.
“Alikuwa anakuja maskani tunakula mambo yetu na hata wakati anafanya kazi kwenye ile Kampuni ya Barrick hapa Dar, ilikuwa kabla hajaenda anapita kwanza huku uswahilini kisha ndiyo anaenda. Kwa maana hiyo malaria ndiyo iliyomuua lakini hata madawa yamechangia.” 
Langa alifariki dunia Juni 13, mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi. Amini!
SORCE: Globalpublishers
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment