LEMA BADO YUPO POLISI MKOANI ARUSHA

.
.
Taarifa za sasa kutoka Arusha ni kwamba Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi Arusha na kuhojiwa kwa tuhuma za uchochezi wa vurugu za Wanafunzi wa chuo cha Uhasibu dhidi ya Mkuu wa Mkoa Arusha juzi.
Taarifa ya wakili wa Lema, Humphrey Mtui ni kwamba Mbunge huyu Polisi imekataa kutoa dhamana yake na kusema mpaka jumatatu ndio itajulikana hatma yake kwenye hii ishu ya uchochezi.
Mbunge Lema alikamatwa jana saa tano na nusu usiku na polisi nyumbani kwake ambapo Polisi walimfata, baada ya kufika kwake walianza kugonga lakini Mbunge huyu alisita kufungua kwa sababu alizotoa kwamba hakua anafahamu watu wanaogonga nyumbani kwake usiku, alianza kupigia simu rafiki zake na watu wake walioanza kukusanyika nje ya nyumba yake.
Muda ulipozidi kwenda polisi walizidi kukusanyika wakiwa na vifaa na mbwa wao pia kitendo kilichofanya baadhi ya marafiki wa Lema kumshauri atoke tu nje ambapo alifanya hivyo na kuchukuliwa mpaka kituoni.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment