KUHUSU WABUNGE WATANO WALIOADHIBIWA KWA KUTOLEWA NJE YA BUNGE KWA SIKU 5

.
Gazeti la Mwananchi, picha inaonyesha Mbunge Lema akizuia askari wasimtoe Tundu Lissu.
Naibu Spika wa Bunge JOB NDUGAI amemtoa nje ya Bunge kwa muda wa siku tano Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni TUNDU LISSU kwa madai ya utovu wa nidhamu na kuanzisha majibizano bungeni kitendo kinachokiuka kanuni za bunge.
Wengine ambao wamepewa adhabu hiyo ya kutohudhuria vikao vya bunge kwa siku tano ni Mbunge wa Mbeya Mjini JOSEPH MBILINYI, Mbunge wa Arusha Mjini GODBLES LEMA, Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji PETER MSIGWA, Mbunge wa Nyamagana EZEKIA WENJE na Mbunge wa Ilemela HIGHNES KIWIA ambao walikuwa wakiwazuia askari wa bunge kumtoa nje LISSU.
Namkariri Naibu Spika akiongea  nje ya bunge akisema “nimemuonya zaidi ya mara kumi kwa jioni ya leo peke yake kwamba demokrasia ya kibunge ni ya kuwapa watu wengine nao nafasi ya kusikika, kila anaesimama anakatishwa yeye kasimama dakika zake zote amekatizwa na kina nani? kinachokosekana kwenye bunge hili ni uvumilivu wa kumsikiliza mwingine, watu wanapenda kumshambulia mwingine lakini hawako tayari kusikiliza wengine wakiwajibu, tunalaumiwa na kila mtu….. hata hatua nilizozichukua ni hatua ndogo tu”

Kabla ya uamuzi wa kutolewa nje ya Viwanja vya bunge haujatolewa, Mbunge wa Iramba Magharibi MWIGULU NCHEMBA ndiye aliyekuwa akichangia Bajeti ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma ambapo namkariri hapa akisema “mimi ni ninachokumbuka labda watu wengine kumbukumbu sijua wanakua na hangover gani, kitu ninachokitambua kwamba Rais amekua mtu wa kwanza kukemea jambo la udini, kuna mgombea wa chama kimojawapo alikua anakwenda anaongea na baadhi ya Viongozi wa kidini kama ndio viongozi na mikutano ya ndani ya chama chake, hili linakubalika wapi? wakari CCM inatumia mabalozi, wenyeviti wa tawi…..”

Mbunge wa Longido LEKULE LAIZER ni kama ametabiri kutokea kwa jambo hilo kabla kwani wakati anachangia amepinga vitendo vya vurugu bungeni hali iliyopelekea kuwakumbuka wabunge wa zamani, namkariri akisema “hivi Mbunge mwenzako anapoongea unaanza kumzomea unafikiria nini? hatujawahi kufikia kiwango hiki”

Sekunde chache kabla ya Naibu Spika kuagiza Tundu Lissu atolewe, alisema “Mh Tundu Lissu sijui ni huu ugeni wa kuwa bungeni, ndio lazima nitoe maoni yangu kama kiongozi… unakuwa wewe ni sehemu ya kufanya vurugu ndani ya bunge? nasema hivi…. askari toa nje Tundu Lissu, askari wakwapi…. toa nje”
Wakati Naibu spika akitoa hilo agizo, wabunge wengine kadhaa walisikika wakisema…. “haiwezekani…… huo ni ubabe…. ubabe ubabe…. polisi, tutoke wote…..” unaweza kuwasikiliza hapa chini..
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment