HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA BALOTELLI KUFUNGIWA


Matukio yamekuwa kama ndiyo rafiki wa karibu wa Mario Balotelli kutokana na mchezaji huyu wa Milan kufungiwa kucheza mechi 3 za ligi ya Serie A, na hii ni kufuatia kitendo chake cha Jumapili cha kumtukana refa aliyekuwa anachezesha mechi yao dhidi ya Fiorentina.

Wakati haya yanampata, Tayari mchezaji huyu alikuwa akose mechi moja kutokana na kadi za njano alizokuwa nazo, na sasa ana mechi mbili zaidi atakazozikosa kwa kumtukana muamuzi msaidizi mwishoni kabisa mwa game.

Haya ndiyo maneno ambayo yamemponza Balotelli ["What the f*** are you looking at?"]

Kwa sasa pia msakata kabumbu huyu anasubiria kulipa faini baada ya kukamatwa akivuta sigara katika choo cha treni waliyokuwa wamepanda na timu yake huko Florence.

Game ambazo Balotelli hatazicheza ni kati ya Milan na Napoli, Juventus na pia catania na kumbuka kuwa kwa mwaka huu mpaka sasa amecheza mechi 11 za klabu na timu ya taifa ambapo 
kati yake ana magoli 10.

SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment