Hii ndio mikakati ya Mwasiti kwa mashabiki wake



 


Moja kati ya mabinti waliowahi kuwika katika muziki wa kizazi kipya Mwasiti Almas, baada ya kuwa kimya kwa muda, hatimaye ameibuka na kuweka bayana kuwa ana vitu viwili vikubwa ambavyo anavifanya kwa ajili ya mashabiki wake.

Katika kufafanua, amesema kwanza, hivi sasa anaandaa album yake ya 3 kwa sababu mashabiki wake wanauliza sana kuhusu album mpya, kutokana na maombi yao ameamua aandae.

Mwasiti alisema ingawa album yake iliyopita iliyoenda kwa jina la 'Kamili' haikumpa mafanikio ya pesa kama alivyotarajia, lakini atafanya album hiyo kwa ajili ya mashabiki wake na pia anataka kuifanyia hiyo album tofauti na album zake zilizopita.

Mwasiti, ambaye anashikilia tunzo mbili za muziki mpaka sasa, huku moja ikiwa kutoka nchi jirani ya Kenya, alieleza utofauti wa album hiyo nikuwepo kwa aina ya muziki ambao ndo muziki anaupenda lakini kutokana na soko la muziki ulivyo anashindwa kuufanya.

Katika album yake mpya itakayokuwa na nyimbo 8 atachanganya nyimbo za mahadhi ya Jazz.

Msanii huyo alisema kuwa kwasasa nyimbo ambazo ziko tayari amefanya katika studio za THT Sound na Ngoma Records, na hajamshirikisha msanii yeyote.

SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment