TAIFA STARS YAFANYA KWELI

Stars ipo nafasi ya pili katika kundi C ikiwa na pointi tatu moja zaidi ya Morocco,Ivory Coast ikiongoza (4) na Gambia ya mwisho. 


Dar. Miaka mitatu imepita tangu CD ya wimbo wa taifa ilipogoma kwenye Uwanja Taifa mbele ya Rais Jakaya Kikwete wakati wa mchezo kati ya Tanzania dhidi ya Morocco.
Sakata la kugoma kwa wimbo wa taifa lilifunika kipigo cha bao 1-0 ilichopata Stars kutoka kwa Morocco, pia Serikali iliagiza matumizi ya ‘brass band’ kwa ajili ya kupigwa nyimbo za taifa kila inapocheza Taifa Stars.
Leo Taifa Stars inashuka kwenye uwanja huo kuivaa Morocco katika harakati zake za kusaka tiketi ya kufuzu kushiriki Fainali za Kombe la Dunia 2014.
Kikosi cha Kim Poulsen kimeonyesha mabadiliko makubwa katika kipindi cha mwaka mmoja kikiwa na rekodi za kuwafunga mabingwa wa zamani wa Afrika, Zambia na Cameroon zote zilifungwa bao 1-0.
Kocha wa Stars, Kim ni dhahiri ataingia uwanjani huku akiwa na matumaini makubwa ya kuwadhoofisha wapinzani wake na kupata ushindi kwani tayari alishaisoma Morocco na kujua ubora na udhaifu ilionao ilipokuwa inashiriki katika Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zilizofanyika nchini Afrika Kusini mapema mwaka huu.
“Nimeiona Morocco katika mechi tatu tofauti kule Afrika Kusini ilipokuwa inashiriki michuano ya Kombe la Afrika. Ni timu nzuri na ina wachezaji wanaocheza soka katika klabu kubwa barani Ulaya, kimsingi nguvu yao ipo katika uwezo wa mchezaji mmoja mmoja, lakini sisi tutacheza kwa umoja zaidi na kuhakikisha tunashinda mchezo wa leo,”alisema Kim.
Naye mshambuliaji Mbwana Samata wa Taifa Stars anaingia kwenye mchezo wa leo akiwa na rekodi nzuri baada ya kuiongoza TP Mazembe kupata ushindi dhidi ya Mochudi nchini Botswana. Pia macho ya mashabiki wengi yatakuwa katikati ya uwanja wakati Abubakari Salum ‘Sure Boy’ na Frank Domayo watapokuwa wakionyesha ufundi wa kugawa pasi fupi na ndefu.
Kikosi: Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Shomari Kapombe, Kelvin Yondan, Agrrey Morris, Frank Domayo, Amri Kiemba, Mwinyi Kazimoto, Mrisho Ngasa, Mbwana Samata na Salum Abubakar.

SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment