Marekani yaonya raia wake wanaoishi Kenya




Kenya

Nchi yakumbwa na hofu ya  kutokuwepo kwa usalama kutokana na kesi inayoendelea
Nairobi. Marekani imetoa onyo kwa raia wake wanaoishi Kenya wajiepushe na mikusanyiko ya umma kutokana na uwezekano mkubwa  wa kuzuka kwa ghasia zitakazotokana na uamuzi wa Mahakama ya Juu unaotarajiwa Jumamosi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ubalozi huo Nairobi, Serikali ya Marekani  iliwaonya raia wake dhidi ya kukaribia mikusanyiko ya watu na kuepuka  maandamano na kuacha kukaa katika  maeneo ya kibiashara yasiyo katikati mwa jiji na mitaa.
Taarifa hiyo ilisema kwamba  wakati wowote panaweza kutokea ghasia wakati Mahakama ya Juu inatarajiwa kutoa uamuzi wa kesi zinazopinga matokeo ya uchaguzi wa urais ifikapo Machi 30.
Huenda kukawa na hisia kali kutoka kwa umma kutokana na uamuzi utakaotolewa,” taarifa hiyo iliyowekwa kwenye tovuti yao Jumatatu ilisema.
“Kumbuka pia mikusanyiko inayonuiwa kuwa ya amani inaweza kugeuka na kuwa ghasia kwa ghafla.” Taarifa hiyo ilizidi kusema kutokana na kuwa uamuzi huo utatolewa wiki ya Pasaka, wanaosafiri kwa mapumziko wanafaa kujitahadhari kwa kuwa huenda kukashuhudiwa misongamano ya magari iwapo ghasia zitaibuka.
“Maandamano huenda yakasababisha misongamano ya magari na kufungwa kwa barabara. Raia wa Marekani  wanashauriwa kufuatilia matangazo ya vyombo vya habari nchini ili wapate maelezo jinsi yanavyochipuka kuhusu maandamano na matatizo ya trafiki.”
Mahakama ya Juu inatarajiwa kutoa uamuzi wake kuhusu iwapo kulikuwa na haki katika matokeo ya uchaguzi wa urais yaliyotangazwa wiki mbili zilizopita na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), ambapo Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi.
Kiongozi huyo wa TNA, aliye kwenye muungano wa Jubilee, alitangazwa mshindi Machi 9, baada ya kupata kura 6,173,433 dhidi ya kura 5,340,546 za  Odinga.
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment