LINAH:SIPENDI KUVAA NGUO NDEFU

Mwimbaji Linah ambae juzi alitangaza  kwamba ameamua kuwazawadia wazazi wake nyumba aliyoijenga Mpiji Mbezi Dar es salaam kwa thamani ya milioni 30 za kitanzania, amesema pamoja na wazazi wake kufahamu kwamba matunda hayo yametokana na muziki peke yake, amekubali kwamba baba yake mzazi mpaka sasa bado hakubaliani na mavazi anayoyavaa Linah.

Namkariri Linah akisema “nimejitahidi sana kuwaelezea wazazi wangu wanielewe litakapotokea tatizo lolote itakua ni bahati mbaya tu lakini sio kwa makusudi, baba anaona pia kwenye magazeti huwa navaa hivi najitahidi kumwambia hivyo ni vitu vya bahati mbaya huwa vinatokea na mimi kama msanii ndio maana tunakula tunaishi lakini ndio kazi”
Mbali  na hayo Linah kasema “nyimbo zangu baba anazisikiliza na anazipenda na anakubali ninaimba kitu ambacho kipo, ila ubishi mkubwa kati yangu na yeye ni mavazi, kuna show na show.. siwezi kwenda kufanya show ufukweni alafu nimevaa magauni, show nyingine tunatakiwa kubang siwezi kuvaa migauni kama niko kanisani”

SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment