Nchi yetu inatumbukia kwenye ufa wa kidini


NILIPOKUWA nikitafakari mjadala wa kuandika kwenye safu hii wiki hii ghafla kukatokea tukio la kusikitisha la kuuawa kwa risasi kwa Padre Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki, Parokia ya Mt. Joseph mjini Zanzibar.
Padre huyo alikuwa akitoka katikati ya mji kwenda eneo la Mtoni Bububu kwa ajili ya kuendesha misa katika Kigango kilichopo eneo hilo, ndipo mauaji yakamkuta akiwa anaingia tu eneo la kanisa.
Tukio hilo la kinyama lilitekelezwa na watu wasiojulikana limeendeleza hofu katika visiwa hivi hasa ikizingatiwa kuwa mwezi Desemba mwaka jana, watu kama hao wakiwa na pikipiki aina ya Vespa walimshambulia kwa risasi Padre Ambrose Mkenda, hali inayoonyesha kuna mkakati wa kushambulia viongozi wa dini visiwani humo.
Tukio jingine ni lile la kumwagiwa tindikali kwa kiongozi wa Kiislamu, Sheikh Fadhil Soraga ambalo pia lilitokea mwaka jana.
Matukio kama haya yanaendelea kushika kasi na kuzua hofu kwa viongozi wa dini huku kila mmoja akijiuliza zamu yake itakuwa lini, hasa ikizingatiwa kuwa Jeshi la Polisi licha ya kuunda vikosi na kuweka mikakati limeshindwa kuwatia nguvuni wanaotekeleza mashambulizi hayo.
Mapema mwaka jana baada ya kujitokeza kwa makundi yanayopinga Muungano yakiongozwa na kundi la Uamsho linalohusisha jumuiya za dini ya Kiislamu, yaliishia na vurugu zilizosababisha makanisa kadhaa kuchomwa moto na kuharibiwa kwa mali za makanisa hayo.
Kwa kifupi, hali ya amani Zanzibar inatia shaka huku udini ukiwa unashika kasi.
Hali hiyo pia imebisha hodi upande wa Bara ambapo vurugu zimezuka katika maeneo mbalimbali.
Hivi karibuni tumeshuhudia machafuko mkoani Geita zilizosababisha kifo cha mchungaji mmoja na watu wengine 10 kujeruhiwa baada ya Wakristo kufungua bucha yao, hali iliyowaudhi Waislamu na kuivamia.
Suala la kuchinja wanyama nalo sasa limechukua hatua mpya baada ya Wakristo nchini hasa Kanda ya Ziwa kudai haki yao ya kuchinja kama wanavyofanya Waislamu.
Katika kujaribu kutatua suala hilo, Waziri Nchi katika Ofisi ya Rais Sera na Uratibu Stephen Wassira na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wamekaririwa wakitaka utaratibu wa Waislamu kuchinja wanyama katika machinjio ya umma uendelee ili kuepusha shari.
Nadhazni suala hili linapaswa kujadiliwa na pande hizo mbili kwa kina ili kutafuta suluhu ya kudumu.
 
SHARE

Milan Tomic

Hi. I’m Designer of Blog Magic. I’m CEO/Founder of ThemeXpose. I’m Creative Art Director, Web Designer, UI/UX Designer, Interaction Designer, Industrial Designer, Web Developer, Business Enthusiast, StartUp Enthusiast, Speaker, Writer and Photographer. Inspired to make things looks better.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment