
Belle 9, aliyejitambulisha kimuziki kupitia vibao
vyake ‘Sumu ya penzi’, Masogange’ na baadaye kudhihirisha uwezo wake na
kibao cha ’wewe ni wangu’ aliweka wazi mipango hiyo katika mahojiano
maalumu na gazeti hili wiki hii.
“Nimeshatuma ‘application’ ya kufanya kazi na
wasanii wa mbele kwa ajili ya kuvuka boda, Casidy ni mwanamziki
ninayemkubali sana, ninachofikiria ni kuufanya muziki wangu kuwa wa
kimataifa,”alisema Belle.
Msanii huyo ambaye jina lake halisi lililopo pia
katika kitambulisho cha Mpigakura ni Abelnego Damian alisema kwamba,
sasa anahitaji kufanya kazi na wanamziki wa kimataifa.
Belle, anayeimba nyimbo zenye vionjo vya kimapenzi
Jumapili iliyopita alizindua nyimbo yake mpya inayojulikana kwa jina
na ‘listen’ alibainisha kuwa mipango anayoitekeleza sasa ya kufanya
kazi na wasanii wa kimataifa aliianza miaka mitatu iliyopita. “Mpaka
sasa nimeshafanya mawasiliano ya kufanya kazi pia na Browman na Sablos
Spire kupitia mawakala wao,”anasema Belle 9.
Anaeleza kuwa juhudi za kuwasiliana na wasanii hao anazifanya kupitia kwa rafiki yake, Johnson Elias anayeishi nchini Australia kwa muda mrefu sasa.
Anaeleza kuwa juhudi za kuwasiliana na wasanii hao anazifanya kupitia kwa rafiki yake, Johnson Elias anayeishi nchini Australia kwa muda mrefu sasa.
“Huyu ndiye anayefanya mipango yote huko, huwa
nawasiliana naye kwa kila hatua anayofikia, sina mashaka kabisa.
Ninachoamini, siku moja nitafanya nao kazi studio,”anasema Belle 9 kwa
matumaini.
Anasema kuwa kwa mujibu wa taarifa anazozipata
kutoka kwa rafiki yake Johnson, maombi yake ya kufanya kazi na wasanii
hao zinamjengea matumaini.
“Johnson ananiambia kuna mazingira magumu kidogo kwa sasa, ila taarifa zangu walizipokea freshi, ila muda mwingi wanabanwa na ratiba za shoo,”anasema Belle 9.
“Johnson ananiambia kuna mazingira magumu kidogo kwa sasa, ila taarifa zangu walizipokea freshi, ila muda mwingi wanabanwa na ratiba za shoo,”anasema Belle 9.
Belle anabainisha vigezo vya kufanya kazi na
wasanii wa kimataifa kuwa ni pamoja na shoo kubwa alizowahi kufanya
msanii awali. “Vigezo vingine wanaangalia kazi na ‘performance’ yako ya
home, wanaangalia unavyokubalika na mashabiki, ninachoamini mashabiki
ndiyo majaji kwangu kuhusu vigezo hivyo,”anasema Belle 9.
Mkakati wa 2013
Belle anasema wakati akiendelea kusubiri ‘colabo’ na wasanii wa kimataifa, mwaka huu pia anatarajia kufanya kazi na wasanii mbalimbali, ambao tayari amefanya nao mawasiliano ya karibu.
“Kuna Wayre, Bebe cool na wengine wengi, ambao nitaandaa kazi kwa ajili ya kufanya nao. Lengo kubwa ni kuhakikisha napanua muziki wangu, kwani sanaa ya bongo haitaweza kutimiza malengo yangu,”anasema Belle 9.
Belle anasema wakati akiendelea kusubiri ‘colabo’ na wasanii wa kimataifa, mwaka huu pia anatarajia kufanya kazi na wasanii mbalimbali, ambao tayari amefanya nao mawasiliano ya karibu.
“Kuna Wayre, Bebe cool na wengine wengi, ambao nitaandaa kazi kwa ajili ya kufanya nao. Lengo kubwa ni kuhakikisha napanua muziki wangu, kwani sanaa ya bongo haitaweza kutimiza malengo yangu,”anasema Belle 9.
Anasema kuwa hatua hizo ameanza kuzitekeleza,
baada ya kufanya colabo na msanii nyimbo za raga’ maarufu kwa jina
Kanball kutoka nchini Kenya
“Nimefanya naye kazi moja inaitwa ‘demu wangu’,
ambayo itatoka hivi karibuni. Ninataka kuitengenezea video ndiyo niitoe,
siwezi kusema itakuwa lini,”anasema Belle 9.
Anabainisha kuwa anatamani siku moja kuingia studio na kufanya kazi na wazalishaji wakongwe (Maproducer) wakiwamo, P Funk Majani, Duke, Timberland na Mona Gangstar.
Anabainisha kuwa anatamani siku moja kuingia studio na kufanya kazi na wazalishaji wakongwe (Maproducer) wakiwamo, P Funk Majani, Duke, Timberland na Mona Gangstar.
Maisha yake
Belle 9 ni mzaliwa wa Iringa mjini miaka 24 iliyopita, ambaye maskani yake iko Morogoro. Mbali na kazi zake nyingi kuzifanyia jijini Dar es Salaam akiwa na bado anaishi maisha ya ukapela.
Anasema kuwa mbali ya muziki, hakuna chochote anachojishughulisha nacho kwa sasa mbali na kazi ya muziki.
Belle 9 ni mzaliwa wa Iringa mjini miaka 24 iliyopita, ambaye maskani yake iko Morogoro. Mbali na kazi zake nyingi kuzifanyia jijini Dar es Salaam akiwa na bado anaishi maisha ya ukapela.
Anasema kuwa mbali ya muziki, hakuna chochote anachojishughulisha nacho kwa sasa mbali na kazi ya muziki.
0 comments:
Post a Comment